JE WAJUA HELA YA MIKOPO KWA ELIMU YA JUU HAINA RIBA

HESLB

HII NDO TAARIFA ILIYOTOLEWA NA MKURUGENZI WA BODI YA MIKOPO MWAKA 2016 @chanzo www.eatv.tv 

FRIDAY , 16TH SEP , 2016

Mkurugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano kutoka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, Cosmas Mwaisobwa amesema Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu pamoja na kwamba inatoa mikopo kwa wanafunzi haitozi riba katika marejesho ya mkopo huo.

Mkurugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano kutoka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, Cosmas Mwaisobwa


Akizungumza Jijini Dar es salaam katika KIKAANGONI ya EATV, Mwaisobwa amesema kwamba Bodi ya Mikopo inachokifanya kwa walipaji ni kutoza tozo ya kulinda thamani ya mkopo ambao mnufaika alichukua.

'Tunatoza kiwango cha asilimia 6 ya tozo ya kulinda thamani ya mkopo kiwango ambacho ni tofauti kabisa na riba, ukiangalia benki kwa sasa hivi kuna ambazo zinatoza zinatoza zaidi ya asilimia 20 hivyo sisi kazi yetu tunasaidia kutoa elimu na siyo kunufaika zaidi” Amesema Mwaisobwa.

Aidha Mwaisobwa amesisitiza kwamba kwa wote ambao walichukua mikopo na wanajificha kukwepa kulipa, ni lazima watalipa kwa kuwa uhakiki kwa sasa hivi unafanyika katika maeneo mbalimbali na wakibainika penati ya asilimia 10 itawahusu wote wanaokwepa na kuongeza kwamba wanaojitokeza kulipa kwa hiari watatozwa asilimia 8% ya pato lao kwa mwezi.

Pamoja na hayo bodi hiyo imewataka wanufaika wa mikopo hiyo kutambua kwamba fedha zinazotakiwa kulipwa ni zote kuanzia za chakula, ada pamoja na fedha za mafunzo kwa vitendo.

SHARE

Author

Hi, Its me Hafeez. A webdesigner, blogspot developer and UI/UX Designer. I am a certified Themeforest top Author and Front-End Developer. I'am business speaker, marketer, Blogger and Javascript Programmer.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment